UA-45153891-1

Wednesday, March 5, 2014

JACKSON KABIRIGI ANAVYOIZUNGUMZIA ‘SWAHILIWOOD’ NA MWELEKEO WA SANAA YA FILAMU NCHINI TANZANIA

Jackson Kabirigi

Jackson Laulent Kabirigi ni muongozaji  wa filamu ‘Director’ aliyeongoza filamu ya ‘Mdundiko’ ambayo imemtangaza sana hapa nchini, Marekani na pande mbalimbali za dunia. Filamu hiyo iliyompa heshima kubwa , iliandaliwa chini ya mradi wa Swahiliwood .

RIHANNA NDANI YA PARIS FASHION WEEK


Tuesday, March 4, 2014

BILL GATES NDIYE NAMBA 1 KWA UTAJIRI DUNIANI 2014

1. Bill Gates
Net Worth: $76 B
Source of wealth: Microsoft   

Kama ilivyo kawaida ya jarida la Forbes kutangaza  kila mwaka watu wanaoongoza kwa utajiri duniani, mwaka huu 2014 anayeongoza ni  Bill Gates wa kampuni ya Microsoft. Hawa ni wengine 9 kukamilisha kumi wa kwanza. 

ELOHOR AISIEN ASEMA ‘GOODBYE’ KWA MASHINDANO YA ‘MISS NIGERIA’

Elohor Aisien
 
Aliyekuwa muandaaji wa shindano ya Miss Nigeria Elohor Aisien chini ya kampuni ya The Elite Model Look, ameachia ngazi na kuachana na uandaaji wa shindano hilo ili kuwekeza nguvu zaidi katika kuandaa matukio ya kifahari zaidi chini ya kampuni yake inayoitwa ‘Prive’. Bi. Elohor Aisien alikabidhiwa haki za ubunifu na utawala na timu ya ‘Miss Nigeria’ July 2012 na kufanikiwa kuandaa shinano la Miss Nigeria 2013 lililowezesha kumpata mrembo Ms Ezinne Akudo.

MAMBO KUMI KUHUSU MWANDISHI WA SCRIPT ZA FILAMU ABDUL SIMBA


Abdul  simba ni mwandishi wa script za fimamu ambaye yuko kwenye mradi wa Swahiliwood  unaofanya  shughuri za utayarishaji wa filamu kwa hisani ya  watu wa Marekani kupitia USAID kwa kushirikiana na kituo cha mawasiliano cha Chuo kikuu cha  John Hopkins pamoja  na Proin Promotions ambao ni wasambazaji wa DVD.Haya ni mambo kumi kuhusu mwandishi huyo:

KARABANI, DJ NA MWANAMUZIKI ALIYEBADILIKA KUWA DIRECTOR WA FILAMU NCHINI TANZANIA

Karabani

“Mwanzoni ilikzuwa kama hobi. Tangu nikiwa mdogonilipenda sana filamu lakini sikufikilia kufanya kazi hii mpaka nilipojihisi kuuchoka  muziki”.  Anasema ‘Director’ huyo ambaye pia ni mtayarishaji wa filamu. Karabani ambaye mwanzoni alikuwa DJ, na baadae mtayarishaji wa muziki, aliona haitoshi na  kuanza utayarishaji wa video za muziki pia. 

CHIMAMANDA ADICHIE AWATAKA WANAHABARI WAMUITE ‘MISS’ BADALA YA ‘MRS’


Mwandishi wa vitabu Chimamanda Ngozi Adichie anayemiliki tuzo nyingi  katika tasnia hiyo, amewaonya  waandishi wa habari nchini Nigeria waache kumuita Mrs Chimamanda Esega, ambapo inasemekana Esega ni jina la ukoo la mume wake, badala yake watumie majina yake wakianza na neno ‘Miss’ yaani Miss Chimamanda Adichie.

Monday, March 3, 2014

LUPITA NYONG’O ASHINDA TUZO YA OSCAR KUPITIA FILAMU YA “12 YEARS SLAVE”



Muigizaji maarufu wa kike wa nchini Kenya ambaye anafanyia shughuri zake za filamu Hollywood nchini Marekani, ameshinda tuzo ya Oscar kwenye tuzo hizo za 86 za Academy kwa uhusika wake katika filamu ya 12 Years a Slave ambayo ilitengenezwa mwaka 2013 chini muongozaji Steve McQueen.

Ameshinda tuzo hiyo kipengele cha ‘Best supporting actress’ ambapo alikuwa anachuana na mastaa wengine wakubwa akiwemo Sally Hawkins wa filamu ya Blue Jasmine na muigizaji maarufu wa nchini Marekani Jennifer Lawrence.


Wednesday, February 26, 2014

KITABU ANACHOSOMA LOVENESS LOVE 'DIVA' KWA SASA


Kuwa mtangazaji, mwandishi  au mwanahabari kwa namna yoyote inakupasa pia kuwa msomaji wa maandiko na vitabu mbalimbali hasa vinavyohusu kipengele husika cha habari  zako. Inaelekea mwanadada huyu alishasoma vitabu vingi na bado anaendelea kusoma.  Kwa sasa anasoma kitabu hiki.

UNGEKUWA 2FACE IDIBIA UNGEJISIKIAJE KWA HILI?


Kweli unapokuwa mtu maarufu jiandae kwa lolote litakalokutokea kuanzia kwenye jamii mpaka vyombo vya habari, hasa mitandao ya kijamii. Jibu la swali hili linaweza kuwa "Vibaya!!!", ingawa naamini kwa  Staa yeyote, jibu linatakiwa kuwa  "Kawaida!!!". Na inabidi litolewe kwa kumaanisha, sio tu kwa sababu linatakiwa kuwa hivyo.