UA-45153891-1

Thursday, December 13, 2012

KALA JEREMIAH KUTOKA NA ALBUM YAKE MPYA

 

Kala Jeremiah baada ya kufanya vizuri katika ngoma yake inayokwenda kwa jina la Dear God, aliweka wazi kwamba siku ya tarehe 20 mwezi huu anatarajia kutoka na album yake mpya inayokwenda kwa jina la Pasaka.Na hapo juu anaonyesha cover yake mpya ya hiyo album.

Monday, December 10, 2012

RAY C AMEPONA: LEO AMEPATA NAFASI YA KUMTEMBELEA RAIS JAKAYA KIKWETE IKULU JIJINI DAR


Mwanamuziki wa Bongo Fleva maarufu kama Ray C siku ya leo amemtembelea Rais Jakaya Mrisho Kikwete ikulu jijini Dar es Salaam na kumshukuru kwa msaada wa matibabu kipindi alipokuwa mgonjwa.
Kwa upande wa mama mzazi wa Ray C amemshukuru sana Raisi Kikwete kwa kuokoa maisha ya mwanaye.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Ray C kushoto ni Mama yake mzazi Ray C Bibi Margareth Mtweve na kulia ni Sarah Mtwere Dada yake Ray C.
Habari kutoka Dj fetty blog 
 

Thursday, December 6, 2012

ALICHOKIANDIKA NONINI KUHUSU PRODUZA P FUNK MAJANI NA PICHA YA MAJANI AMBAYO NONINI AMEIWEKA KWENYE WALL YAKE


Hiyo ni picha ambayo msanii kutoka Kenya Nonini ambaye pia ni mtangazaji alitupia kwenye Wall yake asubuhi,akaambatanisha na ujumbe huuu:
"Producer na mmiliki wa Bongo Records, P.Funk 'Majani',Hakuna msani wa Bongo hajafanya kazi na P- funk pande ya hip hop….Kutoka Kina Proffesor,FidQ,Ngwea na Jaymoe Kimya Kimya....(Huyu ni Daktari Musyoka Wao)"

Monday, December 3, 2012

FID Q AMTAMBULISHA DOGO ALIYEMFUNDA KWA MIEZI 9

 
Mwanamuziki mkongwe wa Hip hop Fid Q , almaarufu kama Ngosha the Don, amesema ameamua kumchukua mwanafunzi mmoja na kumfundisha Muziki ili mwanafunzi huyo aweze kupambana na ushindani mkubwa uliopo kutoka kwa wasanii mbali mbali kwenye Muziki.

Akiongea kupitia kituo kimoja cha Radio leo jijini Dar-Es-Salaam, Fid Q alisema anaona fahari kuwa msanii anayetoa fursa kwa vijana badala ya wao (vijana) kumtegemea kwa kolabo ama pesa lakini kwa kuwafunda yeye mwenyewe wataweza kujihudumia wenyewe katika siku za baadae.

Fid Q amekuwa mfano mzuri sana wa kuigwa katika ubunifu na moyo wa kujitolea, na katika siku za hivi karibuni kupitia mahojiano tuliyoyafanya naye msanii Stamina, alionyesha kumkubali sana Fid Q, na kusema ni mtu anayemtegemgea kwenye Muziki wa Hip Hop kwa sababu anamuona kama ni nguzo na msingi wa Hip Hop hapa bongo.

Stamina alisema “kama kuna msanii ambaye ninamkubali sana, basi ni Fid Q , kwani ni msanii pekee aliyesoma vitabu vingi sana ndiyo maana haishiwi mashairi, pamoja na uwezo wake wa kuchana.
Aidha Fid Q alisema mwanzoni aliwawachukua vijana 6 ambao bado walikuwa hawajakomaa, kwa hiyo akawafanya kama wanafunzi na kuwafundisha muziki, na hatimae sasa mmoja wao amemaliza masomo  na kuwa msanii ambaye aliyeiva kimuziki.

Fid Q alisema “nimeamua kuwafundisha vijana muziki ili wawe na uwezo kama wangu na kuwapa fursa katika maisha yao kwa sababu ni vigumu sana mtu kumpa kazi ambayo itamsaidia kimaisha ila ukimpa fursa utamsaidia sana kuliko kumpa pesa. Alimalizia.

A.Y ASHEREKEA PARTY YAKE NA WATU MBALIMBALI BAADA YA KUPATA TUZO YA CHANNEL "O"


Msanii wa Bongo Fleva almaarufu kama A.Y.baada ya kuwania tuzo ya Channel O Most Gifted East African Award huko nchini South African.
Siku ya jana katika maeneo ya Nyumbani Lounge aliweza kualika ndugu,jamaa na marafiki ili waje kusherekea ushindi wa tuzo hiyo pia bila kusahau mastaa mbalimbali walijitokeza kwa wingi.
                                                           Mchizi Mox,marafiki wa A.y
                                                                      Ommy Dimpoz
                                                       Bonny Love akiwa Mchizi Mox
                                                  Gerry Rhymes,Mchizi Mox na Gk
                                                                 Fm kibonde na A.Y


Sunday, December 2, 2012

Saturday, December 1, 2012

TUDD THOMAS ATOA SIRI YA MAFANIKIO YAKE


Najua nikizungumzia ma producer wakali katika tasnia hii ya muziki hapa bongo basi Tudd thomas atakuwa katika list yangu,sasa leo baada ya kuchonga naye aliweza kunieleza siri ya mafanikio yake katika muziki wa hapa bongo.Alisema kwamba katika maisha yake atosahau kitu kinachoitwa ngoma kwani alieleza hizo ndizo zimemfanya hii leo kujulikana katika tasnia ya muziki na kufanya kazi za wasanii.......... Soma zaidi kwenye Dj Fetty Blog:

Tuesday, November 27, 2012

MSANII SHARO MILLIONEA AFARIKI DUNIA



Msanii wa Bongo movie na mwanamziki Sharo milionea amefariki dunia leo hii kwa ajali ya gari alipokua akielekea Muheza, Tanga., kwa habari zilizothibitishwa na msanii mwenzake wa movie Steve Nyerere, akiongea akiwa katika msiba wa msanii mwingine wa Bongo movie alifariki (John) kwa njia ya simu, akiongea kwa sauti ya masikitiko sana na Dj Fetty alisema
"ni kweli fetty sharo hatupo nae tena na nimeongea na kamanda wa polisi mkoa wa Tanga na kuthibitisha habari hizo"
 akiongea na Clouds Fm, kamanda wa polisi mkoa wa Tanga Bwana Constatine Massawe amesema " kifo cha Millionea kimetokea majira ya saa mbili, eneo linaloitwa Maguzoni songa , akiwa anaendesha gari aina ya toyota Harrier akitokea Dar  kuelekea Muheza, alipofika hapo gari liliacha barabara na kupinduka,na maiti imehifadhiwa katika chumba cha maiti ya  hospitali teule ya Muheza. alikuwa mwenyewe. Mungu ailaze roho ya marehem mahali pema peponi Amen.

Saturday, November 10, 2012

MSHINDI WA EPIQ BONGO STAR SEARCH 2012 NI WALTER CHILAMBO


 
Hawa ndio washiriki watano waliokuwa wamebakia
kutoka katika mchujo tangu ebss 2012 ilipoanza safari yake.
Kutoka kushoto ni  Nsami Nkwabi, Walter Chilambo, Salma Yusuph, Wababa Mtuka na Nshoma Ng'hangasamala            


FAINALI YENYEWE

Kushoto ni washiriki watatu ambao waliingia kumi bora na kulia ni baadhi ya washiriki watatu  ambao walifika hatua ya tano bora.Wakiwa pamoja, ni baada ya kuburudisha kwa wimbo wa pamoja muda mfupi kabla ya fainali ya shindano hilo
Washiriki watano bora wakiwa tayari kuanza kazi, wenye suti ni washereheshaji wa tukio hilo lililofanyika ndani ya ukumbi Diamond Jubilee
 Nsami Nkwabi ndiye aliyefungua dimba akisindikizwa na Barnaba.
 Kila mmoja kwanza alipanda jukwaani na mwanamuziki maarufu kwa kuimba wimbo wa mwanamuziki huyo. Hapa ni Nshoma Ng'hangasamala  akitamba na miondoko ya mwambao wa Pwani.
Salma Yusuph na Linex 
 Wababa na Mwasiti
 Walter na Ditto
 Baada ya Kolabo kila mmoja alisimama kama yeye.Huyu si mwingine bali Nsami Nkwabi !
Baada ya Nsami alifuata Nshoma.Hawa wawili ni mtu na dada yake.
 Salma!!!!!  Msichana mwenye kipaji cha  pekee
 
 Wengine wanamuita "Wafather", wengine "Wadad", huyu si mwingine ni Wababa akiokota mshiko baada ya kuwapa raha mashabiki wake.



Walter  Chilambo  akifanya mambo
 MC’s kijana mtanashati Caesar Daniel na mwana dada mrembo Vanessa Mdee ndio wanasongesha show nzima ya Epiq Bongo Star Search
Majaji wa Epiq Bongo Star Search wakiwa kazini! 
Mashabiki wa Walter wakifanya vitu vyao!
 Na mashabiki wa Wababa kama kawaida!
 Mshindi wa BSS 2010 akitoa burudani
Show ilisindikizwa na burudani toka kwa wasanii  mbalimbali wa muziki wa kizazi kipya
THT Dancers
  Ommy Dimpoz 


 Linah na Amin
 Mzee Yusuph
 Washiriki watatu waliendelea kubaki kati ya hawa
 Salma Yusuph
 Wababa Mtuka
 Walter Chilambo 
 
 Wote wanaweza lakini mshindi lazima apatikane.Mmoja wao aliishia hapa kimashindano
Aimbapo utatamani kumtunza lakini waweza shindwa kutokana na sauti yake nzuri na hisia zitakavyokugandisha kwenye kiti ulichokalia 
 Bila kujali mwanamuziki ni wa jinsia gani,inasemekana shabiki namba moja wa mwanamuziki ni mwanamke, alafu mwanaume anafuata. Wanawake wanashangilia, wanatunza, wanapiga kura. Pamoja na uwezo na sauti nzuri aliyonayo Walter Chilambo,unazani  pia alifanikiwa katika hilo?.Pia nakumbuka maneno ya jaji Master J aliposema,"Walter pamoja na sauti yako nzuri una bahati sketi zinakuzimia, kila la kheri".
 Haya sasa!
Chief Judge wa EBSS Bi. Lita Paursen maarufu kama Madam Lita, akitoa maelezo mafupi kabla ya kumpa CCO wa Zantel nafasi amtangaze mshindi 
CCO wa Zantel ambao ndio wadhamini wa shindano hilo akisubiri kuondoa kiu ya matazamaji. 
Walter Chilambo baada ya kutangazwa mshindi wa EBSS 2012 
Madam Lita akimpoza Salma nakumpongeza kwa hatua nzuri aliyofikia 
 Walter akikabidhiwa zawadi yake ya milion 50Tsh
 Walter akiondoka baada ya kufanya yake