UA-45153891-1

Wednesday, April 2, 2014

DIAMOND PLATNUMZ AZUNGUMZIA KAMPENI YA KILIMO YA ONE.ORG INAYOITWA'Do Agric'


Msanii wa muziki wa kizazi kipya Diamond Platnumz ambaye ni miongoni mwa wanamuziki 19 wa Afrika waliochaguliwa kukutana  nchini Nigeria ili kushiriki katika wimbo wa pamoja wa kuhamasisha vijana kujiunga na kilimo, amesikika akizungumzia kampeni hiyo leo kupitia Clouds FM. 

"Kilimo si ushamba, tajiri wa kwanza Afrika Aliko Dangote ni mkulima pia. Unaweza kuwa na shughuri zako mjini lakini ukawa mkulima pia kupitia watu uliowaajiri ambao wanafanya kazi moja kwa moja shambani, inawezekana pia kwa watu kama sisi ambao wengine wanatuita wauza sura", alisema Diamond ambaye pia akiwa jijini Lagos, amefanikiwa kumalizia wimbo wake anaofanya na staa wa nchini humo 'Iyanya' ambaye alikuwa hapa nchini Tanzania mwaka jana katika msimu wa Fiesta.

MR NICE BADILI MATUKIO HASI KUWA CHANYA



Sina uhakika kama uko facebook, twitter, Insatagram au kwingine niweze hata kushauri chochote kupitia akaunti yako. Labda tu niseme kupitia semadat, sina shaka waweza pata ujumbe huu kupitia watu wengine ambao uko karibu nao na wako mtandaoni. Kaka  umaarufu wako ni mkubwa sana. Mpaka mwanzoni mwa mwaka jana, wewe na  Saida Kalori ndiyo wasanii pekee wa muziki wa Tanzania mliokuwa mkitolewa mifano mpaka na viongozi wataalam wa masoko katika mada mbalimbali za nembo au alama  mashuhuri za watu kwa kuzungumzia mtu mmoja mmoja au kwa lugha ya Kiingereza wanasema 'Personal Branding'.

TUNDAMANI ATAKIWA KUWA MZALENDO


Wakati vyombo kadhaa vya habari vikihubiri Uzalendo na Amani, msanii wa Bongo Flava ambaye kwa sasa anatamba na wimbo wa Msambinungwa, ameonekana kuwa tofauti baada ya mwanadada mmoja anayeitwa Esta kuweka wazi kwamba picha za video ya wimbo huo hazikuchukuliwa  jijini Nairobi kama mwanamuziki huyo alivyosema, bali shughuri hiyo ilifanyika hapa hapa nchini Tanzania kwenye studio inayoongozwa na mwanadada huyo mjasiliamali. 

Tuesday, April 1, 2014

RAMANI YA DUNIA KAMA ILIVYOKUTWA MTANDAONI


BONGO QUEEN LEO NDANI YA SEMADAT

Leo tuko na muimbaji katika muziki wa kizazi kipya yaani  Bongo Flava ambaye anaitwa Linah Sanga. Anatokea katika nyumba ya vipaji THT. Huwezi kuwataja waimbaji bora wa kike nchini Tanzania pasipo kumtaja. Yuko katika tuzo za KTML 2014 kipengele cha muimbaji bora wa kike.

SEMADAT NA WAWILI KWA PICHA- JACKLINE WOLPER NA JOKATE MWEGELO


AGNES GERALD 'MASOGANGE' KUSHIRIKI VIDEO MPYA YA 50 CENT NCHINI MAREKANI


Muigizaji maarufu wa video za muziki 'video vixen' wa hapa Tanzania, Agnes Gerald 'Masogange' ataondoka kwenda nchini Marekani kwa ajili ya kushiriki kwenye video mpya ya mwanamuziki mahiri wa Hip hop nchini Marekani '50 Cent'. Mwanadada huyo ambaye amefanya video za wanamuziki kadhaa wa hapa nchini ikiwa pamoja na za nyimbo kama 'Masogange' wa Belle 9 na 'Nangoja ageuke' wa Mwana FA, ameitwa nchini Marekani kwa ajili ya shughuri hiyo baada ya kuonekana kupitia mtandao wa kijamii wa Youtube kwenye moja ya video za muziki wa Bongo Flava.

Agnes Gerald katika picha zaidi: