UA-45153891-1

Tuesday, May 7, 2013

DIAMOND KUONGEZA IDADI YA MAJINA


TAFSIRI ya neno Diamond kwa kiswahili ni Almasi ambayo ni moja ya madini yenye thamani kubwa. Bila  shaka mwanamuziki Nasibu Abdul “Diamond Platnumz” analitendea haki jina hilo, nalo pia linamtendea haki. Msanii huyo wa Bongo Flava mwenye uwezo mkubwa jukwaani ni miongoni mwa wanamuziki wenye mashabiki wengi Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Mbali na jina hilo, pia anafahamika kama rais wa Wasafi na sukari ya warembo.

Katika pitapita za mitaani, imegundulika kwamba jina lake pia limezaa majina mengine mawili ambayo ni Dai-mond na Dia-mond. Ni majina ambayo yanasikika kutoka kwa baadhi ya mashabiki wake wanaoshindwa kulitamka jina lake vile inavyotakiwa.

Diamond ambaye kwa sasa yuko nchini Uingereza, mwaka huu yuko kwenye tuzo za muziki wa Tanzania “Kilimanjaro Tanzania Music Awards” kwenye vipengere vya msanii bora wa kiume kwa ujumla na msanii bora wa kiume Bongo Flava. 
 Diamond akiwa kazini

No comments:

Post a Comment