UA-45153891-1

Friday, November 22, 2013

DAVIDO ASAIDIA WANAFUNZI NA WATOTO YATIMA KATIKA SIKU YAKE YA KUZALIWA

Davido akiwa na mlezi wa watoto yatima


Siku ya jana Novemba 21, 2013,  ni siku ambayo mwanamuziki wa miondoko ya Afro Pop wa nchini Nigeria anayeitwa David, au  maarufu kama ‘Davido ameongeza mwaka mmoja katika umri wake. Ameitumia  siku yake hiyo ya kuzaliwa kuwatembelea na kuwapa msaada wanafunzi na watoto yatima.

Mwanamuziki huyo ambaye anatarajia kuachia wimbo wake mpya hivi karibuni, aliianzia siku yake katika shule ya msingi ya Ikeja ambayo ni ya serikali ambapo alitoa vifaa vya kufundishia na vifaa vya masomo kwa ajili ya wanafunzi. Baada ya hapo alielekea kwenye vituo cha watoto yatima vya ‘Heart of Gold Children's Hospice’ na  ‘Heritage Homes Orphanage’ ambako alitoa zawadi mbali mbali. Mtandao wa lindaikeji uliandika.

No comments:

Post a Comment