UA-45153891-1

Sunday, November 17, 2013

PETER WA P-SQUARE - BADO YUKO KAZINI INGAWA NI MASAA MACHACHE KABLA YA HARUSI YAKE

Msanii wa P-Square Peter Okoye amekwenda nchini Ghana kutoa burudani kwenye tamasha la “Glo Slide & Bounce” ambalo linafanyika usiku wa kuamkia siku ya harusi yake ambayo ni Jumapili, Novemba 17, 2013. Aliandika kwenye akaunti yake ya twitter kwamba “No bachelor eve for me” akimaanisha kwamba, kwake siku moja kabla ya siku ya harusi siyo ‘issue’ kwa hiyo ratiba zingine zinaendelea kama kawaida.


Peter Okoye akiwa kwenye ndege binafsi ya P-Square

Alisisitiza kwamba atarudi nyumbani pasipo kuchelewa maana kwa kutumia ‘Private Jet (PJ)’ kwa maana ya ndege binafsi, inawezekana bila tatizo. P-Square wanamiliki ndege yao binafsi ambayo hivi punde watatua nayo hapa nchini Tanzania.


Aliyoandika kwenye akaunti yake ya Twitter

 Ndege ya P-Square

No comments:

Post a Comment