UA-45153891-1

Thursday, November 14, 2013

JUHUDI NA KUJITUMA NDIYO SIRI YA MAFANIKIO YA JACKLINE WOLPER

Jackline Wolper

Taarifa kutoka vyombo mbalimbali vya habari ikiwa pamoja na Redio  na  TV kupitia vipindi vya Bongo Movie, zinamzungumzia Jackline Wolper kama  msanii bize kuliko wasanii wote wa kike kwenye tasnia hiyo hapa nchini Tanzania ambaye amefanya na bado ana kazi nyingi zaidi  mwaka huu.

Msanii huyo ambaye anajituma sana na ana historia ya upambanaji mpaka kufikia kufahamika na kukubalika, anaandikwa kwenye magazeti mbalimbali hapa nchini pamoja na mitandao ya kijamii ambayo inazungumzia zaidi kipato chake kupitia Bongo Movies. Taarifa kutoka mtandao wa Vibe zinasema ndiye msanii anayelipwa pesa nyingi kucheza Filamu ambapo kiasi anachopewa kwa kila ‘Movie’ ni zaidi ya shilingi za kitanzania milioni tano.

Jackline Wolper ambaye anajiita Wolpergambe, pia ndiye aliyeshiriki kwenye Filamu nyingi zaidi mwaka huu ambapo kwa mwaka huu pekee, mpaka kufikia Oktoba 20, 2013 alikuwa tayari ameshiriki kucheza Filamu 22.

 Picha za gari la Jackline Wolper aina ya Land Cruiser Prado

No comments:

Post a Comment