UA-45153891-1

Thursday, October 17, 2013

BABA YAKE KANUMBA AINGIA RASMI KWENYE FILAMU

Mzee Charles Kanumba

Baba mzazi wa aliyekuwa muigizaji maarufu wa filamu nchini Tanzania Steven Kanumba, Mzee Charles Kanumba ,ameingia kwenye fani ya uigizaji kikwelikweli na tayari yupo kwenye soko la Bongo Movie baada ya kuigiza kwenye filamu inayoitwa “Mwananjilinji” ambayo tayari imeuza kopi za kutosha kanda ya ziwa.

Amesema anafanya hivyo kwa ajiri ya kumuenzi mtoto wake ambaye vipaji vingi alivyokuwa navyo alivirithi kutoka kwake. Alipoulizwa ana vipaji gani, kupitia Amplifier ya Clouds FM, amesema yeye ni muimbaji wa kwaya  muda mrefu sana, mpiga gitaa, muigizaji na mchekeshaji ambaye amekuwa akiyafanya yote hayo kwenye shughuri za kanisa.

Amesisitiza kwamba wapenzi wa filamu wakae mkao wa kula na watarajie makubwa sana kutoka kwake.

No comments:

Post a Comment