UA-45153891-1

Wednesday, October 23, 2013

DIVA ATAMANI COLLABO LA SHILOLE NA IYANYA

Loveness Love 'Diva'

MTANGAZAJI  wa Clouds FM Loveness Love 'Diva' ametamani ufanyike wimbo wa kushirikiana kati ya mwanamuziki wa Bongo Flava na Filamu 'Shilole' na Mwanamuziki wa Nigeria 'Iyanya'. "Natamani Iyanya afanye collabo na Shilole maana staili zao za muziki zinafanana", alisema Diva kwenye kipindi chake cha 'Ala za roho' Octoba 21, 2013 huku wimbo unaotamba Afrika wa mwanamuziki Iyanya, unaoitwa 'Kukere' ukichezwa redioni. 

Shilole ambaye siku chache zilizopita alisikika akisema ana mpango wa kurekodi wimbo na Jenifer Lopez wa nchini Marekani, anafanya vizuri na wimbo wake mpya wa 'Nakomaa na jiji' na ataungana na wasanii wengine wa Bongo Flava kwenye tamasha la Fiesta litakalofanyika Jumamosi ya Oktoba 26,2013 katika viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam.

Iyanya anakuja nchini Tanzania kwa ajiri ya tamasha hilo na ataungana na wasanii wengine kutoka nje ambao ni 'Davido' wa Nigeria, 'Mohombi' wa Sweeden, 'Alaine' wa Jamaica na wengine.

Shilole na Iyanya

No comments:

Post a Comment