UA-45153891-1

Thursday, October 10, 2013

FAHAMU UBUNIFU NA HISTORIA YA MASOUD KIPANYA KATIKA SANAA YA UCHORAJI NA HABARI

Masoud Kipanya

Msanii Ali Masoud maarufu kama ‘Masoud Kipanya’ ambaye kwenye ukurasa wake wa facebook anajitambulisha ‘Political Cartoonist’ kama kazi yake ya kwanza, anajulikana kama mchora katuni maarufu nchini na  mtangazaji wa redio na TV ambaye aliwai kufanya kazi kwenye kituo cha redio cha Clouds FM. Jina lake lilitokana na muonekano wa katuni anayotumia, wenye sura ya panya. Mbali na shughuri hizo pia ni mbunifu katika fani ya mitindo na mtayarishaji wa vipindi.

Alizaliwa tareha 23 Juni 1972 jijini Dar es salaam na kuanza kazi hiyo ya sanaa akiwa shule ya msingi. Kazi yake ya kwanza ilichapishwa kwenye jarida la Heko mwaka 1989, baada ya hapo alifanya kazi kama mhariri wa katuni kwenye gazeti la Sanifu na mhariri mtendaji wa katuni gazeti la majira, pia katuni zake hutokea gazeti la Mwananchi.

Ameshiriki maonyesho mbalimbali Tanzania na Afrika Kusini kama mtaalam wa matumizi ya rangi ‘Painter’ na amejishindia tuzo nyingi ikiwa pamoja na tuzo ya kwanza ya katuni Afrika Mashariki. Pia alishiriki mashindano ya sanaa ya uchoraji yaliyoandaliwa na Friedrich Ebert Stiftung na kupata nafasi ya kutembelea nchini Japan kwenye program ya wiki mbili ya maonyesho ya kimataifa ya utamaduni yaliyoandaliwa na ‘Japan Foundation’.

Ndiye mbunifu wa vipindi vya Televisheni vya ‘Maisha Plus’ na ‘Inawezekana’ pamoja na taasisi binafsi ya  ‘Inawezeka Foundation’. Pia ni CEO wa kampuni ya KP Media.

Kufahamu wachoraji wengine wa katuni, tembelea: bongotoons

Masoud Kipanya Cartoon  @facebook.com



6 comments:

  1. Thank you for the sensible critique. Me and my neighbor we were doing some research about this but will never find a useful and nice information like the ones will saw on your website . I think I learned more clear from this post. I am very glad to see such wonderful info being shared freely out there.one thing i should let you know, your way of
    writing skill has motivate me to start my own blog now.you can click to see all the package i have for you and please don't fail to write me back. thanks for all your effort.

    ReplyDelete
  2. Kaka nina cha kukwambia lakini sjui nakupataje!

    ReplyDelete
  3. Kaka nina cha kukwambia lakini sjui na kupata wapi

    ReplyDelete