UA-45153891-1

Friday, September 27, 2013

FAHAMU MASHINDANO 5 YA UREMBO YENYE UMAARUFU MKUBWA DUNIANI

WAKATI wadau, wapenzi na mashabiki  wa  Urembo na Mitindo ulimwenguni wakingoja nani atatangazwa mshindi wa Miss World 2013 na atatoka nchi gani kesho Septemba 28, fahamu mashindano 5 ya urembo yanayoongoza kwa kufahamika zaidi Ulimwenguni.

1. MISS WORLD

Hili ndilo shindano kubwa kuliko yote ulimwenguni lilianzishwa mwaka 1951 nchini Uingereza na mjasiliamali Erick Morley akiwa na mke wake Julia Morley. Ndilo shindano lenye umaarufu kushinda yote na linalotangazwa na vyombo ya habari vingi ulimwenguni. Kwa mwaka huu litafanyika Septemba 28 jijni Bali, nchini Indonesia. Nchi ya Tanzania inawakilishwa na Brigitte Alfred.
                                                Miss Tanzanai 2012- Brigitte Alfred.

    
  2. MISS UNIVERSE
 
Hili ndilo shindano linalofuatia baada ya MissWord. Lilianzishwa mwaka 1952 nchini Marekani na kampuni ya mavazi ya Pacific Mills jimboni Calfornia kabla ya kumilikiwa na Donard Trump. Lilibadilishwa jina kutoka Miss Universe Inc na kuitwa Miss Universe Organization mwaka 1998 na makao yake makuu yakaamishwa kutoka  Los Angeles, California, kwenda New York . Kwa hapa Tanzania, aliyeshinda mwaka jana (2012) kushiriki mashindano hayo ni Winfrida Dominic.
 Miss Universe Tanzania 2012-Winfrida Dominic.

    3. MISS INTERNATIONAL
Ni shindano la urembo lililoanzishwa nchini Marekani mwaka 1960 jimboni California na kuhamishiwa jijini Tokyo nchini Marekani ambako ndiyo makao makuu yake.Mwaka 2011, Tanzania iliwakilishwa na mrembo Nelly Kamwelu ambaye pia kwa mwaka huo huo alishiriki mashindano matatu kuiwakilisha Tanzania, ambayo ni Miss Universe Tanzania ,Miss Southern Africa International na  Miss International 2011.

 Miss International Tanzania-Nelly Kamwelu

4. MISS EARTH
4.   Ni miongoni mwa mashindano makubwa manne ya urembo duniani. Lianzishwa mwaka 2001 na liko chini ya Miss Earth Foundation. Lilianzishwa kwa ajiri ya kuhamasisha utunzaji wa mazingira na mshindi wa shindano hilo ndiye msemaji wa Miss Earth Foundation na shirika la uratibu wa shughuri za mazingira la umoja wa mataifaHYPERLINK "http://en.wikipedia.org/wiki/United_Nations_Envi(UNEP) na mashirika mengine ya mazingira. Aliyeshinda mwaka 2012 kuiwakilisha Tanzania kwenye shindano hilo ni Bahati Chando.
    Miss Earth Tanzania 2012- Bahati Chando.

        5. MISS TOURISM (MISS UTALII)
Ni miongoni mwa mashindano maarufu ya urembo ulimwenguni, Kwa mara ya kwanza Tanzania ilifanya vizuri katika shindano hilo ambapo mshiriki Nelly Kamwelu ambaye alikuwa mshindi wa 5.  Aliyeshinda  mwaka 2012 kuiwakilisha Tanzania kwenye shindano hilo ni Hadija Saidi Mswaga.
 Miss Tourism Tanzania 2012/2013-Hadija Saidi Mswaga.

No comments:

Post a Comment