UA-45153891-1

Tuesday, September 10, 2013

GARI ALILOTOA DIAMOND KWA MZEE GURUMO LINAONGEA



Mzee Gurumo na Diamond siku ya tukio hilo

Kwanza pongezi nyingi zimuendee msanii wa muziki wa kizazi kipya Diamond Platnumz kwa kitendo alichofanya siku chache zilizopita wakati akizindua video mpya ya wimbo wake wa “Number one”.Pia shukurani zenye ujazo wa kipekee zimuendee Mzee Gulumo kwa kuweka wazi, kwani hakakulenga kumkatisha mtu tamaa aliposema anastaafu bila hata baiskeli, bali kutoa changamoto kwa wanamuziki na sekta nzima inayohusu Sanaa. Hakika wanamuziki hawa ni hamasa ya ubunifu.
Baada ya kutafakali kitendo hicho, kwa mtazamo wangu, zawadi aliyotoa Diamond inazungumza mambo mengi kwa watu tofauti.

Wadau wa sanaa na wafanyabiashara
Kutowasahau wasanii wazee, wao pia wana umaarufu mkubwa na wakipewa nafasi kushiriki kampeini mbalimbali na matangazo wanaweza kufanya vizuri katika nafasi zao (Celebrity endorsement)

Wasanii wakongwe
Wasanii wakongwe na hasa wa kizazi kipya wajenge tabia ya kuwaheshimu na kuwapa moyo wasanii wanaochipukia hii inafanya wao pia waheshimike mara kumi zaidi ya kawaida. Nakumbuka usiku flani msanii Chris Brown alikuwa akifanya onyesho kwenye tuzo flani za muziki nchini Marekani. Justine Timberlake alipopata nafasi ya kuuzungumzia usiku huo alisema yafuatayo ukumbini “When I see Chris Brown on stage, it reminds me on how much I getting old”.Kwamba amuonapo Chris akifanya vitu vyake jukwaani inamkumbusha jinsi gani yeye anaanza kuzeeka. Ni mara chache sana kwa hapa Bongo kusikia maneno kama haya.

Wasanii wanaochipukia
Kujiandaa kustaafu. Wafanyakazi walioajiriwa kwenye sekta rasmi huanza kujiandaa kustaafu baada tu ya mwezi wa kwanza tangu wanapoanza kazi kupitia mifuko mbalimbali inayohifadhi kiasi flani cha mshaara. Mbinu tofauti inaweza kutumika kwa kila msanii ikiwa ni pamoja na kuwekeza. Kutobweteka na kuvimba vichwa mambo yanapowanyookea. Wakumbuke pia kwamba siku za nyuma sanaa ilikuwa haijaanza kulipa kama sasa kutokana kutokuwapo kwa utayarishaji bora wa kazi, uchache wa vyombo vya habari, uchache wa matumizi ya sanaa na wasanii kwenye matangazo ya biashara, udhamini na mengine mengi. 

Mashabiki
Kununua kazi halali za wasanii pasipo kudurufu itasaidia sana kuongeza kipato cha wasanii.
 Diamond akimkabidhi Mzee Gurumo gari

No comments:

Post a Comment