UA-45153891-1

Saturday, September 21, 2013

"TATIZO NINI? BEI YA MKAA", "WATUACHE TULALE"!

MANENO na misemo mingi inayoingia na kukaa kwenye vichwa vya watu na hasa watoto na vijana ambao ndiyo wengi, hutokana na nyimbo za wanamuziki, waigizaji kupitia kazi zao, matangazo maarufu ya biashara na maneno au kauli za watu wengine maarufu (Quotations) ikiwa ni pamoja na viongozi.

Kila wiki siku ya Jumamosi, Semadat blog itakuwa ikikuletea kilichozungumzwa mtaani na mtu yeyote kwa kuweka msisitizo au akizungumza katika hali ya utani kwa kutumia maneno au misemo hiyo.

Kwa kuanza, leo amekutwa kijana mmoja maeneo ya kona ya barabara ya kwenda Chuo kikuu cha Dar es Salaam jirani na Mlimani City jijini Dar es Salaam, ambaye ameonekana akiwa na mawazo mengi. Alipoulizwa "TATIZO NINI?", jamaa mmoja pembeni akajibu kwa utani "BEI YA MKAA". Baada ya dakika kadhaa akashuka dada mmoja kutoka kwenye  Bajaji akiongea kwa njia ya simu kwa sauti ya juu, maongezi ambayo ni kama alikuwa anapinga jambo flani. Ghafla akamalizia kwa kusema "WATUACHE TULALE", akaweka simu yake mfukoni na kuondoka.


"Week End" njema na endelea kutembelea SEMADAT (Hamasa ya Ubunifu).

Nick wa pili  " Bei ya mkaa"
Joe Makini
Diamond "Watuache tulale"

No comments:

Post a Comment