UA-45153891-1

Monday, September 30, 2013

MICHUZI-FAMILIA YA ‘BLOGGERS’ NCHINI TANZANIA

Muhidin Issa Michuzi akizungumza jambo kwenye moja ya makongamano
                              

UKITEMBELEA mtandaoni utakutana na  neno  'Michuzi' kwa majina mengine tofauti na Issa Michuzi mmiliki wa Michuzi Blog. Ni Blogs au maarufu kama Blogu zinazomilikiwa na watanzania wengine wanaotokea katika familia moja na Blogger huyo mkongwe Muhidin Issa Michuzi.

Safari yake ilianza kwa kupenda kazi ya kupiga picha na kusomea fani hiyo miaka ya 80. Akiwa anaendelea na shuguri zake, siku flani  moja ya picha zake ikachaguliwa kuingia kwenye ukurasa wa mbele wa  gazeti la serikali la Daily News , akaendelea  kufanya kazi na gazeti hilo na kisha kuajiriwa kabisa na chombo hicho cha habari mwanzoni mwa mwaka 1990. Baadae aliongeza taaluma ya ‘Photojournalism’ mjini Berlin na  uandishi wa habari  Chuo kikuu cha Dar es Salaam na kumaliza mwaka 1996.

Alianza kazi ya Blogu  mwaka 2005 ambapo kwa mara ya kwanza Blogu yake iliingia mtandaoni Septemba 8, 2005. Lengo lake kuu ikiwa ni kuwapa watu habari zinazohusu nchi ya Tanzania kupitia Blogu ya picha “photoblog.

Mpaka sasa anamiliki tuzo nyingi ikiwa ni pamoja na Blogu inayoongoza Tanzania kutoka ‘1st Annual Tanzanian Blog Awards’,  Blogu bora ya habari za siasa mwaka 2011 kutoka ‘VADE Local Digital Media’ na ‘Vodacom Awards for Digital Excellence’ mwaka 2012.

Ndugu zake ambao pia wanafahamika kama Bloggers ni Ahmad and Othman na pamoja wameanzisha kampuni ya habari ambayo inaitwa Michuzi Media Group (MMG).
.

No comments:

Post a Comment