UA-45153891-1

Saturday, September 28, 2013

MISS PHILIPPINES MEGAN YOUNG ACHUKUA TAJI LA MISS WORLD 2013


 MISS WORLD 2013-Megan Young wa Philipines

Megan Young wa Philipines ndiye aliyenyakua taji la shindano la Miss World 2013, lililofanyika Bali Indonesia leo Septemba 28, 2013.

Ameandika kwenya ukurasa wake wa facebook kwamba aliteleza na kuanguka kabla hajapanda stejini kwenye shindano la Top Modal.  Aliongeza kwamba hakutegemea angeshinda kutokana  na kwamba si mrefu akijilinganisha na washiriki wengine walivyokuwa.” Kwa kufikiria hilo la kutokuwa mrefu, imenifanya niongeze juhudi zaidi kuutafuta ushindi”.Ameandika  Megan Young, Miss World 2013.

Shindano limemalizika huku Miss Brazil Sancler Frantz akichukua tuzo ya Miss Beach Beauty, Miss Netherlands Jacqueline Steenbeek akichukua tuzo ya  Miss Sportswoman, Miss India Navneet Kaur akiondoka na tuzo ya Miss Multimedia  pamoja na  Miss Nepal Ishani Shrestha kunyakua tuzo ya Miss Beauty with a Purpose.

                     Miss Brazil Sancler Frantz aliyechukua 'Miss Beach Beauty Award'
Miss Netherlands Jacqueline Steenbeek aliyechukua ' Miss Sportswoman Award
 Miss India Navneet Kaur aliyechukua  Miss Multimedia Award
Miss Nepal Ishani aliyechukua Miss Beauty with a Purpose Award
 Washiriki wakati wa shindano la Miss Word 2013 leo Sept 28,2013

No comments:

Post a Comment