UA-45153891-1

Wednesday, September 25, 2013

MWANAMUZIKI WA KENYA ANNETTE KAWIRA ALIVYOPONEA CHUPUCHUPU KWENYE TUKIO LA UGAIDI LA 'WESTGATE MALL'

                                                               Annette Kawira

MWANAMUZIKI  chipukizi wa nchini Kenya Annette Kawira ambaye anaendelea kupata umaarufu kutokana na wimbo alioshirikishwa na Nonini ambao unaitwa Pole pole, ni miongoni mwa waliokuwa kwenye jengo la biashara la Westgate nchini Kenya wakati likivamiwa na kutekwa na Alshabab.

Ni muda mfupi tu mama yake alikuwa amefika nyumbani akitokea hapa nchini Tanzania. Alimsalimia mama yake kwa furaha na  kumwambia wataongea mengi baadae maana alikuwa tayari amechelewa kazini. Alijiandaa,  akamuaga mama yake, akumbusu mdogo wake wa kiume, kisha akaanza safari kuelekea 'Westgate Mall'.

Anasema alipokuwa ndani ya jengo hilo, akasikia risasi ya kwanza na kuzani ni Transfoma, jambo lililofuata ni kuona mtu mmoja amedondoka chini na damu nyigi zikimtoka. Alianza kuwaza mengi juu ya familia yake na hasa mama yake ambaye akupata hata nafasi ya kuongea nae kabla hajaondoka. Milio ya risasi ilipozidi kuongezeka akaona ndiyo mwisho wake huku akiwaza ni kitu gani kitaandikwa juu ya kumbukumbu yake.

Annette hakupata madhara yoyote isipokuwa mtu mmoja ambaye anafanya nae kazi.Anamshukuru Mungu kwa kumuepusha na anawaombea wote ambao bado wako katika hali ngumu wapate kukombolewa.

No comments:

Post a Comment