UA-45153891-1

Thursday, September 26, 2013

GORAN TOMASEVIC, MPIGA PICHA WA KIMATAIFA NA MWANDISHI WA HABARI ZA KIVITA ALIVYOFANYA KAZI KWENYE TUKIO LA ‘WESTGATE MALL’ NCHINI KENYA

Jengo la Westgate likiwa tayari limetekwa

Kama umekuwa ukifuatilia tukio la kigaidi la nchini Kenya kufuatia uvamizi na utekaji wa Jengo la 'Westgate Mall' utakuwa umekutana na picha za kipekee (exclusive photos) zilizochukuliwa ndani ya jengo hilo wakati uokoaji ukiendelea. Aliyekuwa akifanya yote hayo nyuma ya Kamera si mwingine bali Goran Tomasevic. Ni mwandishi wa habari upande wa upigaji wa picha ambaye ni mkongwe mwenye uzoefu wa miaka 20. Anashughurika na matukio ya hatari hasa yale ya kivita. Kwa muda huo amekuwa mpiga picha kwenye migogoro mbalimbali ikiwemo ya Afghanistan, Iraq, Libya, Misri na Syria. Kwa sasa anafanyia kazi nchini Kenya.

Mpiga picha Goran Tomasevic

Ifuatayo ni stori  fupi aliyoitoa kuhusu tukio la Westgate," Nilikuwa nyumbani niliposikia kutoka kwa rafiki yangu mmoja kwamba kuna jambo limetokea japo wote hatukuwa na uhakika ni kitu gani, Tulienda mpaka maeneo ya jengo la Wastage Mall na kuona baadhi ya miili imelala maeneo ya kuegesha magari, basi hapo nikagundua hili si jambo la kawaida.  Niliona baadhi ya askali wa Kenya wakiwa wamejificha pembeni mwa magari nami nikafanya hivyo, huku nikisogelea mlango wa kuingilia, kisha nikaona askali wengine wengi na kuwauliza ni muda gani wataingia ndani, wakaniambia muda huo huo wanaigia ndani ya jengo kupitia juu. Nami nikaigia nao ndani ili kuchukua picha. Pia niliwasaidia askali kwenye baadhi ya matukio ya kuwakomboa mateka".
Zifuatazo ni baadhi ya picha alizopiga nje na ndani ya jengo hilo.



No comments:

Post a Comment