UA-45153891-1

Monday, September 23, 2013

LEO DUNIANI: TAMASHA LA MWISHO LA BOB MARLEY



SIKU ya leo, wanamuziki wa Reggae, mashabiki wa muziki huo na wapenzi wa muziki kwa ujumla, wanaikumbuka siku ya mwisho kufanya tamasha la muziki ya gwiji wa miondoko hiyo hayati Bob Marley. Tarehe ya Septemba 23, 1980, Bob Marley alifanya tamasha la mwisho 'Bob Marley's last ever concert'ndani ya Stanley Theatre, Pittsburgh kabla hajarudi nyumbani Jamaica kumalizia muda wake wa mwisho baada ya matibabu ya maradhi ya saratani yaliyokuwa yakimsumbua kutofanikiwa.

Alifariki dunia Mei 11, 1981 akiwa na umri wa miaka 36 na maneno ya mwisho aliyaongea kwa mtoto wake Ziggy akisema ‘Money can’t buy life.’yaani pesa haiwezi kununua maisha. Albam yake ya 'Exodus'ilitajwa na jarida la 'Times' kama albam bora ya karne ya 20. Kwa muda mfupi alioishi duniani, alitambulika ulimwengu mzima na muziki wake ukabaki kama alama ya maisha yake na kipaji chake.

No comments:

Post a Comment