UA-45153891-1

Monday, January 27, 2014

BABY MADAHA AENDELEA KUTENGENEZA 'HEADLINE' NCHINI KENYA


"Sexy Tanzanian Singer Admits Top Kenyan Record Producer is ‘More Than a Manager to Her". Ndivyo ulivyoandika mtandao maarufu nchini humo unaoitwa 'Ghafla' .

Baby Madaha akiwa na Joe

Muimbaji na muigizaji wa kike ambaye ni zao la Bongo Star Search, Baby Madaha, amekubali kwamba ana uhusiano wa kimapenzi na meneja wake ambaye pia ni mtayarishaji wake 'Producer' wa label ya Candy n Candy, Joe Kariuki. Ni baada ya siku chache zilizopita kuandikwa na mitandao mbalimbali ya Tanzania juu jambo hilo.

Akihojiwa na jarida la 'Spice' la nchini humo, Baby alisema, " Uhusiano wangu na Joe, mmmmh.... Joe amekuwa ni zaidi ya msimamizi wa kazi zangu. Natumia  muda wangu mwingi nikiwa na yeye, sijari watu wanasema nini. Ninafurahi na kama uhusiano wangu na Joe hauniathili kwa namna yoyote kwa nini nitazame wengine. Kama yuko 'single' kuna tatizo gani akiwa na mimi?"

Baby Madaha anafanya vizuri na wimbo wake wa 'Summer holiday' chini ya  studio za  Candy n Candy nchini Kenya.

No comments:

Post a Comment