UA-45153891-1

Thursday, January 23, 2014

D'BANJ ATAMBULIWA RASMI NA MTANDAO WA FACEBOOK (VERIFIED)

'Facebook page' ya  D'Banj ndivyo inavyoonekana

Ukurasa wa Facebook wa mwanamuziki maarufu wa Nigeria D'Banj 'Kokomaster', staa wa Oliver twist, imehakikiwa na kuthibitishwa na mtandao huo kwa kuwekewa alama ya 'tick' ya rangi ya Bluu, hivyo kuitofautisha na zile zilizofunguluwa kienyeji na watu wangine kwa kutumia jina lake.

D'Banj anakuwa mtu wa pili nchini humo ambapo kabla ya hapo aliyekuwa na ukurasa wa Facebook katika hali hiyo ya kutambuliwa ni Rais wa Nigeria Goodluck Jonathan peke yake.

Tofauti na kwenye mtandao wa Twitter ambao watu wengi maarufu nchini humo wana alama hiyo, kwa upande wa Facebook si kitu rahisi na kwa hapa nchini Tanzania hakuna aliyewekewa alama hiyo kwenye Facebook japo upande wa Twitter wapo kama Rais Kikwete,  AY, January Makamba, Flaviana Matata na Hasheem Thabeet.

No comments:

Post a Comment