UA-45153891-1

Wednesday, January 22, 2014

MWAFRIKA MWEUSI WA KWANZA KUTEMBEA NJE YA SAYARI YA DUNIA

Mandla Maseko

Anaitwa Mandla Maseko.Ni Dj wa mtaani,nchini Afrika Kusini, mwenye umri wa miaka 25, akitokea wilaya ya Mabopane jirani na jiji la Pretorea.Ni baada ya kushinda mashindano yaliyoandaliwa na wanataaluma wa anga wa nchini Marekani.Amewashinda washiriki zaidi ya milioni moja kutoka nchi 75 na kuwa mmoja wa watu 23 watakaotembelea mwezini.

Alikuwa mwanafunzi wa Uandisi wa Ujenzi (Civil Engineering) ambaye alisitisha masomo baada ya kushindwa kulipa ada.Bado anaishi na wazazi wake na ndugu zake wanne ambapo katika familia yake hakuna hata mmoja ambaye alishatoka nje ya Afrika Kusini. Katika hali ya kawaida inasemekana  kutembelea huko ni gharama zisizopungua dola za kimarekani 100,000.

No comments:

Post a Comment