UA-45153891-1

Tuesday, January 21, 2014

RAIS OBAMA ALIPOSEMA BANGI HAINA MADHARA MAKUBWA ZAIDI YA POMBE


Akinukuliwa na gazeti la New Yorker linalotoka Jumapili,alipofanyiwa usaili kuhusiana na mjadala wa uhalalishaji wa Bangi katika maeneo ya Washington na Colorado,  Rais Obama alisema "Nilishavuta nikiwa mdogo na ipo kwenye historia. Hii ni tabia mbaya kama ambavyo pia nilivuta sigara. "Ila sizani kama ni hatari kuliko pombe". 

"Si hatari zaidi ya pombe?", aliulizwa Rais Obama. Hata hivyo alielezea anachokimaanisha kuwa si kwamba anaunga mkono matumizi yake bali hafurahishwi na masuala ya sheria  inayowatolea macho na kuwafunga kwa muda mrefu watoto wa masikini kutokana na mazingira ambayo yanawafanya waonekane, wakati watoto wa familia za maisha ya kati na wa matajiri wakitumia na kuendelea kupeta.

No comments:

Post a Comment