UA-45153891-1

Saturday, January 25, 2014

KUHUSU VIDEO YA "TEMA MATE TUWACHAPE", MADEE NA BARAZA LA SANAA LA TAIFA (BASATA)

Kufuatia mitazamo tofauti ya kimaadili na kiutamaduni juu ya video ya muziki, ya wimbo wa "Tema mate tuwachape" ambayo ni ya msanii wa Bongo Flava maarufu kama Madee, kumekuwa na tetesi kwamba Basata wamempigia simu Madee kuzungumza nae juu ya suala la hilo.

 Madee
Hata hivyo msanii huyo amesema kupitia Planet Bongo ya East African Radio kwamba baada ya kupigiwa simu alizungumza na msimamizi wake na kuambiwa angoje barua kwa sababu anaweza kuwa mtu binafsi kaamua tu kutumia jina la chombo hicho kuzungumza anavyotaka au kuzingua kama wanavyosema watoto wa mjini.

Hivyo video hiyo inaendelea kupeta na itazidi kupeta pasipo kujali maneno ya watu na kama kuna lolote chombo husika kitamtaarifu Madee kwa maandishi. Hii ni kwa mujibu wa maelezo aliyoyatoa staa huyo wa wimbo wa "Pombe yangu".

No comments:

Post a Comment