UA-45153891-1

Sunday, January 26, 2014

MILLARD AYO ASHEREHEKEA SIKU YAKE YA KUZALIWA AKIWA DUBAI

Mwandishi wa habari na mtangazaji wa Clouds FM Millard Ayo anasherehekea siku yake ya kuzaliwa leo Januari 26, 2014 akiwa Dubai. Mtangazaji huyo maarufu kama 'Mr.Count down', anayesikika kupitia kipindi cha 'Amplifaya',  alizaliwa siku au tarehe kama aliyozaliwa kocha maarufu wa soka Jose Mourinho.

Staa huyo ambaye ni miongoni mwa watanzania wenye wafuasi wengi kwenye mitandao ya kijamii, amesikika redioni akizungumzia siku hii na pia ameandika kupitia mtamdao wa Instagram kwamba uwepo wake ndani ya Dubai ni zawadi kutoka kwa bosi wake Joseph Kusaga.

No comments:

Post a Comment