UA-45153891-1

Friday, January 24, 2014

FAHAMU JINA LA AINA YA NDEGE ANAYOTUMIA MSAANII 'JAGUAR'

 Jaguar

Ni kawaida sana watu kutaka kujua mtu flani maarufu anatumia usafiri gani kama ni 'mkoko' ni gari gani na aina gani, mfano Mercedes benz SL300, Toyota Altezza AS200, Audi TT na nyinginezo.Lakini tunapokuja katika suala la ndege, hapo wengi huishia kusema ndege.Hata hivyo inatosha kutokana na hadhi ya chombo hicho japo baadhi hupenda kufahamu zaidi.

Ndege ya Jaguar aina ya Cessna

Ndege anayotumia msanii Jaguar wa nchini Kenya ni aina ya Cessna. Japo haijajulikana ni Cessna toleo gani maana kuna Cessna 205, 206, 207, 310 na zingine lakini ni aina ya ndege iliyotengenezwa na Kampuni ya Cessna ambapo toleo la kwanza lilitoka mwaka 1962 na mpaka kufikia mwaka 2006 zilikuwa tayari zimetengenezwa ndege 8509 za aina hiyo. Ni aina ya ndege inayotumika kibiashara na safari binafsi. Bei ya ndege hizo ni kati ya dola za kimarekani laki tisa ($900,000) mpaka milioni 26 ($26,000,000).

Jaguar anaitumia ndege yake kibiashara na si kwa matumizi binafsi.

No comments:

Post a Comment