UA-45153891-1

Friday, January 24, 2014

MASHABIKI WA JUSTIN BIEBER WAANZA KUPOTEZA IMANI NAE


Ni baada ya kukamatwa na polisi kwa tukio lililomtia hatiani kwa makosa ya kuendesha gari akiwa amelewa pombe, matumizi ya madawa ya kulevya, leseni iliyoisha muda wake na  kuendesha  mwendo wa  kasi kwa shinikizo. Alikamatwa pamoja na muimbaji aliyejulikana kama Khalil Amir Sharieff baada ya askali kuwaona wakiendesha magari flani ya bei mbaya katika hali ya mashindano.

Justin Bieber akipigwa pingu

Justin Bieber mwenye umri wa miaka 19 ambaye ana ushawishi mkubwa kwa vijana wadogo kupitia sanaa ya muziki na  mwanamuziki anayefuatwa zaidi na watu wengi kwenye mitandao ya kijamii, mashabiki wake wametoa maoni yao kupitia mitandao hiyo ambapo wengi hawajafurahishwa na matukio hayo na kusema anapoteza muelekeo. Baadhi yao wanashauri apate muongozo mzuri  ili hasipotee zaidi.

No comments:

Post a Comment