UA-45153891-1

Friday, January 24, 2014

BABA MZAZI WA MARY J. BLIGE AUMIZWA NA MPENZI WAKE WA ZAMANI


Baba yake na mwimbaji mashuhuri wa RNB, Mary J. Blige, ameripotiwa kuwa yuko katika hali mbaya baada ya kuumizwa shingo kwa kuchomwa kisu na 'X-girlfriend' wake katika ugonvi wa nyumbani. Taarifa zinasema tatizo limeanza baada ya baba  huyo anayeitwa Thomas Blige mwenye umri wa miaka 63 kumshambulia mpenzi wake kwa maneno kwamba ametoboa magurudumu ya gari lake.
Mary J. Blige

Mwanamke aliyefanya tukio hilo lililotokea majira ya asubui Alhamisi ya January 23, 2014 anashikiliwa na Polisi. Thomas Brige ambaye kwa sasa amelazwa hospitali, inasemekana zamani alikuwa mwanamuziki wa Jazz na ni veterani wa jeshi. Aliondoka na kumuaacha Mary J.Blige akiwa na miaka minne.

Inasemekana ndiyo maana katika wimbo wa Mary J. Blige unaoitwa 'Father in you', mwanadada Mary alishuka mistari "When I was a little girl / I didnt have a father / And that's why I'm learning on you/".

No comments:

Post a Comment