UA-45153891-1

Tuesday, March 4, 2014

MAMBO KUMI KUHUSU MWANDISHI WA SCRIPT ZA FILAMU ABDUL SIMBA


Abdul  simba ni mwandishi wa script za fimamu ambaye yuko kwenye mradi wa Swahiliwood  unaofanya  shughuri za utayarishaji wa filamu kwa hisani ya  watu wa Marekani kupitia USAID kwa kushirikiana na kituo cha mawasiliano cha Chuo kikuu cha  John Hopkins pamoja  na Proin Promotions ambao ni wasambazaji wa DVD.Haya ni mambo kumi kuhusu mwandishi huyo:

1.    Ana miaka kumi sasa tangu aanze kufanya kazi hiyo.

2.    Alijifunza mwenyewe kwa kuwa alipenda sana kuandika stori na alitumia muda wake mwingi kuatazama filamu za aina mbalimbali. 

3.    Ndoto  ilianzia alipotamani kukibadilisha kuwa filamu kitabu cha ‘Things Fall Apart ‘ kilichoandikwa na mnigeria Chinua Achebe.

4.    Amesomea mambo ya  Historia, Siasa na Falsafa nchini Uingereza.

5
.    Dira yake kuu ni kuwaenzi waandishi  wa Tanzania na  Afrika nzima kwa kufanya kazi zao zikumbukwe kupitia filamu.

6.    Alipata hamasa kubwa kutoka kwa dada yake ambaye pia alikuwa kwenye sanaa ya muziki ,filamu na uandishi wa vitabu.

7.    Hatua ya kwanza ilianzia mwaka 2004 pale alipopata nafashi kushiriki kwenye ‘Maisha Screen Lab’ jijini Kampala, chini ya Muongozaji wa filamu wa nchini India ‘Mira Nair’ ambaye alimwambia anaweza kuandika.

8.    Anaiona gharama ya teknolojia kama changamoto  kubwa kwenye utayarishaji na matumizi ya filamu.

9.    Ameandika Script  ya  filamu ya Sunshine, moja  ya filamu mpya kutoka Swahiliwood.

10.   Mama  yake ni mchanganyiko wa kichaga na kisomali  na baba yake mchanganyiko wa Kigoma na Rufiji.


1 comment:

  1. Shkamooo...nataka kuusajili mswada Wangu kabla ya kuuza-je! Ni lazima? Kama ni lazima /muhimu: nasajilia wapi? Tafadhali nijibu.
    goodbeatus92@gmail.com

    ReplyDelete